Kombe la Dunia 2026: “Sijafurahishwa na Mchezaji Wetu – Kwa Kila Kitu” - Kocha wa England
Kocha wa England, Thomas Tuchel, amekiri kutofurahishwa na kiwango cha mchezo wa timu yake katika ushindi wa kushtua dhidi ya Norway kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia.
Tuchel amesema Three Lions walicheza kwa uzembe, na ushindi wao umepatikana kibahati tu ila hawakuwa katika kiwango cha mchezo kinachotakiwa “kwa kila hali” licha ya kufuzu hatua ya nusu fainali.
“Tumebahatika,” alisema Tuchel baada ya mchezo ambao Norway ilitangulia kufunga, ikakosa nafasi kubwa ya kuongeza bao la pili, ikakataliwa bao jingine na pia kupiga mpira uliogonga mwamba wa goli.
“Tumefanya mambo kuwa magumu sana kwetu wenyewe. Matokeo ni mazuri. Tumefika hatua ya nusu fainali. Ni jambo la kufurahia, lakini sijafurahishwa na uchezaji wetu — kwa kila hali.
“Tumefanya maisha kuwa magumu kupitia namna tulivyocheza. Tumecheza kwa uzembe, tumefanya makosa mengi ya kiufundi, hatukuwa na kasi ya kutosha na hatukuwa na mwendelezo wa kutosha.”
Tuchel amesema kuna jambo moja lililosaidia England kufuzu hatua inayofuata.
“Hii ni nguvu ya akili na dhamira ya timu,” amesema kocha huyo.
Soma zaidi: