“Labda Tuchel hajui ilivyo kucheza na wachezaji kama Haaland – Bellingham amjibu Tuchel
Kauli ya kocha wa England, Thomas Tuchel, kwamba timu yake “inapaswa kucheza vizuri zaidi” huenda haikuwa maneno ambayo shujaa wa mchezo huo, Jude Bellingham, alitaka kuyasikia baada ya kipenga cha mwisho.
Kiungo huyo wa Real Madrid alivaa jezi namba 10 na kuonyesha kiwango kikubwa cha nguvu katika mchezo uliodumu dakika 120, uliochezwa kwenye joto kali na hali ya unyevunyevu kupita kiasi, akisaidia England kufuzu hatua ya nusu fainali ya Kombe la Dunia.
Juhudi hizo za aina yake zimefikiwa chini ya wiki moja baada ya wachezaji hao hao wa England, wakiwa pungufu kwa mchezaji mmoja, kufanya kazi ya ziada ya ulinzi na kuichapa Mexico katika uwanja wake wa Azteca kwenye hatua ya 16 bora.
Kauli ya Tuchel kwamba England ilishinda kwa “nguvu ya akili” lakini “inapaswa kucheza vizuri zaidi” ilimfanya Bellingham kuitikia kwa kutikisa mabega.
“Ndiyo, ni sawa, vyovyote vile,” alisema Bellingham katika mahojiano yake baada ya mchezo kwenye uwanja mjini Miami.
“Hali ni ngumu kule, ni kazi kubwa sana. Wachezaji wote wamejituma kupita kiasi. Mawazo yangu na shukrani zangu zinaenda kwa wachezaji waliopambana na kufanya kazi ya ziada,” amesema Bellingham.
“Labda yeye (Tuchel) hajui ilivyo kucheza katika mazingira kama yale dhidi ya wachezaji kama Erling Haaland, Martin Odegaard, Antonio Nusa na Alexander Sorloth,” Bellingham aliongeza:
“Si timu rahisi kucheza nayo. Sifa zote nawamiminia wachezaji wenzangu.
“Huwezi kushinda kila mchezo kwa kupiga pasi nyingi na njia bora. Wakati mwingine lazima ushinde kwa kupambana na kwa njia ngumu, na ndivyo tulivyofanya leo.”
Soma Zaidi: