Helikopta zagongana Brazil; Mwanamuziki wa Marekani afariki dunia

Chanzo cha picha, Getty Images
Helikopta mbili zimegongana nchini Brazil na kusababisha kifo cha mwanamuziki mashuhuri wa Marekani Oliver Tree miongoni mwa watu sita.
Moja ya helikopta imeanguka kwenye maegesho ya muuzaji wa magari na kusababisha karibu magari 20 kuwaka moto.
Picha zilizochapishwa na vyombo vya habari vya Brazil zinaonyesha moja ya helikopta ikidondoka kutoka angani, huku miali ya moto na moshi mzito ukipanda kutoka eneo la ajali.

Chanzo cha picha, Getty Images
Mwanamuziki aliyeaga dunia mwenye umri wa miaka 32 alikuwa kwenye ziara ya ulimwengu wakati ajali hiyo ilipotokea huko Rio de Janeiro siku ya Jumapili.
Mamlaka zinasema uchunguzi kuhusu chanzo cha ajali hiyo unaendelea.
Idara ya Kijeshi ya Zimamoto ya Jimbo la Rio de Janeiro ilisema iliitwa kwenye eneo la ajali karibu 09:00 saa za eneo (12:00 GMT).
Mtengenezaji maudhui kutoka Argentina Gaspar Prim Diaz - anayejulikana kama Gaspi - pia anaaminika kuwa katika mojawapo ya helikopta hizo, kulingana na chombo cha habari cha Associated Press.
Oliver Tree Nickell alizaliwa huko Santa Cruz, California mnamo mwaka 1993 na alipata umaarufu kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2016 baada ya kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Soma zaidi:






















