Msafara wa mazishi ya Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran waanza mjini Tehran
Msafara wa mazishi ya Kiongozi Mkuu wa zamani wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, umeanza safari yake kupitia mji mkuu, Tehran.
Khamenei aliiiongoza Iran kwa zaidi ya miaka 35 kabla ya kuuawa katika mashambulizi ya anga yaliyotekelezwa na Marekani na Israel mwezi Februari.
Mazishi yake yalianza Ijumaa na yatafanyika kwa kipindi cha siku saba, yakihusisha shughuli mbalimbali katika maeneo ya Iran na Iraq. Mamlaka za Iran zimesema kuwa kati ya watu milioni 12 na 20 wanatarajiwa kushiriki katika hafla hizo za mazishi.
Mrithi wa Khamenei, mwanawe Mojtaba Khamenei, hadi sasa hajaonekana hadharani katika mazishi ya baba yake, licha ya kuhudhuriwa na viongozi kadhaa waandamizi wa utawala wa Iran.
Uvumi kuhusu hali ya Mojtaba umeendelea kuenea, ukichochewa na taarifa zisizothibitishwa kuwa alijeruhiwa katika mashambulizi hayo hayo ya Marekani na Israel yaliyomuua baba yake.
Hajajitokeza hadharani tangu ateuliwe mapema mwezi Machi.