England yaichapa Mexico katika mechi ya kusisimua na kutinga robo fainali
Uingereza ilionesha mchezo wao bora zaidi katika Kombe la Dunia huku kukiwa na shauku na hisia katika Uwanja wa Azteca na kupata ushindi mkubwa dhidi ya Mexico uliowasaidia kutinga robo fainali dhidi ya Norway.
Huku mechi ikicheleweshwa kwa saa moja kutokana na dhoruba kali, kikosi cha Thomas Tuchel kilinusurika kadi nyekundu ya Jarell Quansah mapema kipindi cha pili na kurekodi moja ya ushindi wao bora zaidi katika miaka ya hivi karibuni.
Mexico ilikuwa imepoteza michezo miwili tu kati ya 89 ya ushindani katika ngome yao ya Azteca, lakini mbinu ya Uingereza ya mapema iliwaruhusu kuongoza wakati Jude Bellingham alipofunga mabao mawili katika sekunde 98 kabla ya mapumziko.
Mlinda lango wa Uingereza Jordan Pickford alikuwa katika hali nzuri sana, akiokoa mara mbili kwa ustadi mpira kutoka kwa Raul Jimenez, lakini hakuwa na nguvu ya kumzuia Julian Quinones akifunga bao la kurudisha kwa Mexico.
Sauti za mara kwa mara za kelele, ziliongezeka wakati Quansah alipotolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya Jesus Gallardo, lakini Uingereza ilirejesha uongozi wao wa mabao mawili wakati Harry Kane alipofunga kwa penalti baada ya Anthony Gordon kuangushwa na mlinda lango Raul Rangel.
Wakati tu Uingereza ilipofikiri wamerejesha utulivu, Kane alimchezea visivyo Brian Gutierrez katika eneo la hatari, Jimenez akifunga penalti. Wakiwa na shinikizo na katika hali ya wasiwasi, Tuchel aliwaingiza Dan Burn na Djed Spence, wakirejea kwenye ulinzi wa wachezaji watano na kupata ushindi wa dakika 11 za mwisho.
Unaweza kusoma;