Mbappe aweka rekodi ya mfungaji bora Ufaransa
Ufaransa imekuwa na idadi kubwa ya wachezaji mahiri wa kushambulia kwa miaka mingi lakini hakuna bora zaidi katika ufungaji magoli kuliko Kylian Mbappe baada ya kufunga mabao yake katika mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia dhidi ya Senegal.
Mshambuliaji huyo wa Real Madrid amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Ufaransa, akimpita Giroud katika rekodi ya mabao aliyofungia Les Bleus ikiwa ni bao lake la 58 akiwa na umri wa miaka 27 tu.
"Hongera Kylian," Giroud alisema kwenye BBC One, akiwa kama mchambuzi wa mchezo wa Ufaransa dhidi ya Senegal. "Ninamfurahia."
"Inaeleweka, ilitarajiwa. Atavunja rekodi zote - idadi ya mechi na mabao. Nadhani anaweza kufikia mabao 100 kwa urahisi na labda [kuvunja] rekodi ya Miroslav Klose ya Kombe la Dunia. Amekuwa na matokeo mazuri katika Kombe la Dunia na michezo mikubwa."
Mabao ya Jumanne yalimfanya afikishe mabao 14 katika Kombe la Dunia - mawili tu nyuma ya Klose wa Ujerumani, ambaye anashikilia rekodi hiyo akiwa na mabao 16 ambayo nayo pia sasa imefikiwa na Lionel Messi.
"Anajua anakotaka kwenda, ni kiongozi na hilo lilionekana tangu akiwa mdogo. Ni mchezaji mwenye kipaji cha ajabu na nadhani ni kiongozi mzuri ndani na nje ya uwanja."
Soma zaidi: