Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Iran na Marekani zaonya Israel dhidi ya kushambulia Lebanon

Makao makuu ya jeshi mjini Tehran yamesema Israel imekiuka makubaliano hayo mara 84 katika kipindi cha siku mbili zilizopita.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Mbappe aweka rekodi ya mfungaji bora Ufaransa

    Ufaransa imekuwa na idadi kubwa ya wachezaji mahiri wa kushambulia kwa miaka mingi lakini hakuna bora zaidi katika ufungaji magoli kuliko Kylian Mbappe baada ya kufunga mabao yake katika mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia dhidi ya Senegal.

    Mshambuliaji huyo wa Real Madrid amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Ufaransa, akimpita Giroud katika rekodi ya mabao aliyofungia Les Bleus ikiwa ni bao lake la 58 akiwa na umri wa miaka 27 tu.

    "Hongera Kylian," Giroud alisema kwenye BBC One, akiwa kama mchambuzi wa mchezo wa Ufaransa dhidi ya Senegal. "Ninamfurahia."

    "Inaeleweka, ilitarajiwa. Atavunja rekodi zote - idadi ya mechi na mabao. Nadhani anaweza kufikia mabao 100 kwa urahisi na labda [kuvunja] rekodi ya Miroslav Klose ya Kombe la Dunia. Amekuwa na matokeo mazuri katika Kombe la Dunia na michezo mikubwa."

    Mabao ya Jumanne yalimfanya afikishe mabao 14 katika Kombe la Dunia - mawili tu nyuma ya Klose wa Ujerumani, ambaye anashikilia rekodi hiyo akiwa na mabao 16 ambayo nayo pia sasa imefikiwa na Lionel Messi.

    "Anajua anakotaka kwenda, ni kiongozi na hilo lilionekana tangu akiwa mdogo. Ni mchezaji mwenye kipaji cha ajabu na nadhani ni kiongozi mzuri ndani na nje ya uwanja."

    Soma zaidi:

  2. Kombe la dunia 2026: Messi afunga magoli matatu yake ya kwanza huku wakiipa Algeria kichapo

    Lionel Messi amekuwa mfungaji bora wa muda wote wa Kombe la Dunia kwa kufunga mabao 3 huku mabingwa watetezi Argentina wakianza kwa kupata ushindi dhidi ya Algeria.

    Messi akicheza mechi yake ya 200 kwa nchi yake alitengeneza historia, kwani mshindi huyo mara nane wa Ballon d'Or alifikisha jumla ya mabao yake ya fainali za Kombe la Dunia hadi 16 - na kumfanya awe sawa na Miroslav Klose wa Ujerumani kama mfungaji bora wa wakati wote katika historia ya mashindao hayo.

    Mabingwa hao mara tatu wa dunia walilazimishwa kutafuta ushindi kwa bidii ili wawe kifua mbele katika Uwanja wa Kansas City huku wakilenga kuwa taifa la tatu pekee kutetea Kombe la Dunia kwa mafanikio.

    Ilikuwa mara ya kwanza kwa Argentina kushinda mechi yao ya ufunguzi kwenye Kombe la Dunia kama mabingwa watetezi, baada ya kushindwa mwaka 1982 na 1990.

    Hilo lilitokana na weledi wa Messi, ambaye alifunga bao la ufunguzi la kuvutia dakika ya 17.

    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 alipokea mpira kutoka kwa mchezaji mwenzake wa Inter Miami, Rodrigo De Paul, kabla ya kumchenga Luca Zidane - mtoto wa gwiji wa Ufaransa, Zinedine Zidane - katika mechi yake ya 27 ya Kombe la Dunia.

    Bao lake lilifungwa dakika 12 baada ya juhudi za awali kukataliwa wakati wa mwanzo mgumu, huku Algeria pia ikipata shuti lililokataliwa dakika tatu baadaye huku mchezo ukianza kwa kasi tangu mwanzo.

    Lakini usiku ambao alikuwa mchezaji wa kwanza kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya sita, Messi alikuwa na bahati ya kuepuka adhabu kwa kumchezea vibaya Aissa Mandi wa Algeria katikati ya kipindi cha kwanza.

    Bao la pili la Argentina lilifungwa kwa karibu sana katika dakika ya mwisho wakati Messi alipomrukia Zidane kimakosa, kabla ya kufunga mabao matatu ya kwanza ya Kombe la Dunia katika dakika ya 76 kwa shuti kali kutoka ukingoni mwa eneo la hatari baada ya kuchukua mpira kutoka kwa Nicolas Gonzalez.

    Baada ya kuanza kwa ushindi katika Kundi J, Argentina itakabiliana na Austria na Jordan.

    Soma zaidi:

  3. Iran na Marekani zaonya Israel dhidi ya kushambulia Lebanon

    Iran imeitaka Israel kusitisha mara moja mashambulizi yake kusini mwa Lebanon, ikitishia kutoa "kujibu vikali" iwapo uvunjifu wa makubaliano ya kusitisha mapigano utaendelea.

    Makao makuu ya jeshi mjini Tehran yamesema Israel imekiuka makubaliano hayo mara 84 katika kipindi cha siku mbili zilizopita.

    Kwa upande mwingine, Rais wa Marekani Donald Trump ametoa kauli nzito akikosoa mbinu za kivita za Israel dhidi ya Hezbollah.

    Rais Trump ameeleza kutoridhishwa na kitendo cha Israel kubomoa majengo ya ghorofa kwa ajili ya kutafuta mtu mmoja, akisisitiza kuwa raia wengi wanaopoteza maisha si wapiganaji wa Hezbollah.

    "Ikiwa Israel haiwezi kufanya operesheni yake bila kuua kila mtu, basi Syria itafanya kazi hiyo," Trump alisema.

    Katika pendekezo la kushangaza, Rais Trump amedokeza kuwa ni bora kuiachia Syria jukumu la kushughulikia kundi la Hezbollah, akiamini kuwa inaweza kufanya kazi hiyo kwa ufanisi zaidi bila kusababisha vifo vingi vya raia.

    Shinikizo la kimataifa dhidi ya operesheni za kijeshi za Israel limefikia kilele huku kukiwa na mgogoro wa kidiplomasia kuhusu hatua za kijeshi nchini Lebanon na Gaza.

    Soma zaidi:

  4. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara. Tarehe ni 17/06/2026.