Zelensky amshutumu Putin kwa kukataa amani na kuchelewesha mipango ya vita
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, ameikosoa Urusi kwa kuendelea na vita, akisema Moscow imekuwa ikiahirisha mipango yake ya kijeshi na kukataa mapendekezo yote ya amani yaliyowasilishwa ili kumaliza mzozo huo.
Kwa mujibu wa Reuters, Rais Volodymyr Zelensky, amesema Kremlin imeweka na kuahirisha mara 15 muda wake wa kujitwalia eneo la mashariki la Donbas katika kipindi cha zaidi ya miaka minne ya vita.
Kauli za Zelensky zilikuwa jibu kwa matamshi ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ambaye siku moja kabla alikuwa amekataa kile alichokitaja kuwa pendekezo la Ukraine la kusitisha mashambulizi ya masafa marefu na kupunguza mapigano.
Soma zaidi;