Morocco yatinga 16 bora kwa penalti

Chanzo cha picha, Getty Images
Michuano ya Kombe la dunia imeendelea kushuhudia matokeo ya kushtua baada ya Morocco kutinga hatua ya 16 bora kwa kuiondoa Uholanzi kwa mikwaju ya penati kufuatia sare ya 1-1 iliyodumu hadi baada ya dakika 120.
Morocco sasa imeungana na Brazil, Canada na Paraguay katika hatua ya 16 bora, ikivunja rekodi ya Uholanzi ya kutofungwa na timu ya Afrika katika michuano hiyo.
Katika mechi nyingine ya kusisimua, mabingwa mara nne wa dunia Ujerumani wameaga mashindano hayo baada ya kufungwa na Paraguay kwa mikwaju ya penati 4-3, kufuatia sare ya 1-1 iliyodumu hadi mwisho wa dakika 120.
Ujerumani haikuwahi kupoteza mechi kwa penati kwenye kombe la dunia.
Mshambuliaji wa Arsenal, Kai Havertz, pamoja na mshambuliaji wa Newcastle United, Nick Woltemade, walikosa penati zao baada ya kudakwa na kipa wa Paraguay, Orlando Gill.
Maelezo zaidi:

