Moja kwa moja, Marekani na Israel zinajiandaa kushambulia tena Iran -ripoti

Kwa mujibu wa vyanzo vilivyonukuliwa na CBS, Rais wa Marekani Donald Trump bado hajatoa amri ya mwisho ya kuanzishwa kwa mashambulizi hayo.

Muhtasari

Ruka Video uendelee
  • xx
  • Besigye
  • .
  • xx
  • xx
  • xx
  • Lungu
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi

  1. Askofu Mkuu wa Canterbury awasili Cameroon kwa ziara ya kichungaji

    .

    Chanzo cha picha, MINAT

    Askofu Mkuu wa Canterbury, Dame Sarah Mullally, amewasili nchini Cameroon kwa hatua ya pili ya ziara yake ya mataifa mawili barani Afrika.

    Hapo jana alipokelewa na viongozi wa serikali ya Cameroon, maafisa wa Kanisa la Anglikana pamoja na Kamishna Mkuu wa Uingereza nchini humo.

    Akiwasili katika uwanja wa ndege wa Yaoundé, alisema anafurahia kutembelea taifa hilo la Afrika ya Kati katika ziara yake ya siku kumi barani humo.

    "Ni heshima kubwa kwangu kuwa hapa Cameroon. Hii ni mara yangu ya kwanza kutembelea Afrika kama Askofu Mkuu wa Canterbury," aliwaambia waandishi wa habari.

    Aliongeza kuwa yuko nchini humo kwa ziara ya kichungaji ya kuomba, kuabudu pamoja na Kanisa la Anglikana, kutembea bega kwa bega na waumini wake, na kuwatia moyo katika huduma yao.

    Kabla ya kuwasili nchini humo, Dame Sarah alikuwa Ghana kwa siku tano ambapo alikutana na waumini wa Kanisa la Anglikana na kuimarisha uhusiano wao na Kanisa la England.

    Akiwa huko pia alithibitisha tena dhamira ya kanisa hilo ya kutenga pauni milioni 100 katika mfuko wa kushughulikia athari za kihistoria za ushiriki wa Kanisa la England katika biashara ya utumwa kupitia Bahari ya Atlantiki.

    Katika ziara yake ya siku tano nchini Cameroon, atatembelea miji minne, ikiwemo Buea na Limbe katika eneo la Kusini Magharibi linalozungumza Kiingereza, ambako mgogoro wa mapigano umeendelea kwa karibu muongo mmoja.

    "Katika kipindi hiki cha migogoro mikubwa duniani na mateso yanayoendelea hapa Cameroon, nimekuja nikiwa na ujumbe wa Injili," alisema, akieleza kuwa ujumbe huo ni wa amani.

    Akiwa Buea, atatembelea taasisi inayotoa mafunzo kwa wauguzi na wakunga. Uhusiano wake na taaluma ya uuguzi unatokana na kazi yake ya awali kama muuguzi katika Huduma ya Afya ya Taifa ya Uingereza (NHS), ambako alipandishwa vyeo hadi kushika nafasi za juu.Siku ya Jumapili, Askofu Mkuu huyo mwenye umri wa miaka 64 atahubiri katika Bishopscourt jijini Douala, makao makuu ya Dayosisi ya Cameroon. Pia atatembelea makanisa mbalimbali na kukutana na viongozi wa dini katika jiji hilo.

    Atakaporejea Yaoundé siku ya Jumatatu, atatembelea taasisi nyingine za kidini na kufanya mazungumzo na viongozi wa serikali kabla ya kuondoka nchini Cameroon siku ya Jumanne.

  2. Maafisa tis wa Ukraine wauawa katika shambulizi la Urusi mjini Kyiv

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Takribani watu tisa wameuawa katika mashambulizi ya makombora ya balistiki ya Urusi dhidi ya Ukraine, kwa mujibu wa maafisa wa eneo hilo mapema Jumamosi.

    Watu wengine 23 walijeruhiwa katika shambulio hilo dhidi ya mji mkuu, Kyiv, kulingana na Huduma yaDharura ya Ukraine.

    Moscow imeongeza mashambulizi ya makombora ya balistiki maafa dhidi ya mji mkuu wa Ukraine, jambo lililomfanya Rais Volodymyr Zelensky kusema kuwa mifumo ya kuzuia makombora inahitajika kwa dharura.

    Mashambulizi hayo yalifanyika siku mbili baada ya kombora la kurushwa kutoka kwa 'meli' linalodhaniwa kuwa la Urusi kuangukia nchini Poland wakati wa shambulio kubwa dhidi ya Ukraine lililoua angalau watu wanane, wakiwemo wanafamilia sita wa familia moja katika kijiji kilicho karibu na Kryvyih Rih.

    Meya wa Kyiv, Vitali Klitschko, alisema mji mkuu huo ulishambuliwa kwa makombora ya balistiki, huku shirika la habari la AFP likiripoti milipuko zaidi ya 10.

    Moto ulizuka katika maeneo mbalimbali ya jiji na kukatika kwa umeme kuliripotiwa katika baadhi ya maeneo.

    Klitschko alisema jengo la makazi katika eneo la Shevchenkivskyi liliharibiwa kwa kiasi, na kuacha watu wakiwa wamenaswa ndani.

    Huduma za dharura zilisema angalau watu saba waliuawa katika shambulio katika wilaya ya Darnytskyi. Watu wengine 14 walijeruhiwa, wakiwemo watoto wawili, iliripoti huduma hiyo.

  3. Kifaa kisichojulikana kilichorushwa kutoka angani chagonga meli ya mafuta karibu na Oman

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Shirika la Operesheni za Biashara ya Baharini la Uingereza (UKMTO) limetangaza kuwa meli ya mafuta imegongwa na kifaa kilichorushwa ambacho hakikutambuliwa, umbali wa kilomita 20 kaskazini-mashariki mwa Lima, Oman.

    Kulingana na afisa usalama wa mmiliki wa meli hiyo, mgongano huo uliharibu chumba cha injini na meli hiyo haiwezi tena kuongozwa wala kuendelea na safari yake. Walinzi wa pwani katika eneo hilo wamearifiwa na mamlaka zinafanya uchunguzi kuhusu shambulio hilo.

    Hakuna ripoti zozote za majeruhi au madhara kwa mazingira kufikia sasa. UKMTO imezitaka meli zinazopita eneo hilo kuwa waangalifu na kuripoti shughuli yoyote ya kutiliwa shaka.

    Tukio hili linakuja wakati ambapo mvutano wa masuala ya baharini umeongezeka katika maji yanayozunguka Iran na Oman; katika wiki za hivi karibuni, meli kadhaa za kibiashara zimeshambuliwa katika Ghuba ya Oman na karibu na Lango la Bahari la Hormuz.

    Wakati huo huo Iran imeweka vikwazo vya usafiri katika Lango la Bahari la Hormuz, huku Marekani ikituma vikosi vyake vya majini katika eneo hilo, ikisema inachukua hatua kulinda uhuru wa usafiri wa baharini.

    Bado haijabainika ni nani aliyehusika na shambulio dhidi ya meli hiyo ya mafuta.

    Soma zaidi hapa:

  4. FIFA yafuta mpango tata wa uwekezaji wa Kombe la Dunia

    Gianni Infantino

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Gianni Infantino, anasema amefuta mpango uliozua utata wa kuuza hisa katika mashindano makuu ya shirikisho hilo, kufuatia upinzani mkubwa.

    Raia huyo wa Uswizi alisema ni wazi kuwa mradi huo "umesababisha migawanyiko" ambayo "haiendani tena na maslahi" ya lengo lake la awali.

    Raia huyo wa Uswizi aliongeza: "Kwa sababu hiyo, mpango huu hautaendelezwa."

    Infantino alikuwa ameahidi kutoa dola milioni 40 kwa vyama vyote 211 wanachama iwapo vingeliunga mkono pendekezo la kuanzisha kampuni tanzu ya biashara kusimamia mashindano yake makubwa, ikiwemo Kombe la Dunia, na kuruhusu wawekezaji wa nje kununua hisa katika kampuni hiyo.

    Rais wa Shirikisho la Soka la Asia (AFC), Sheikh Salman bin Ebrahim Al Khalifa amekaribisha hatua ya kufutwa kwa mpango huo.

    "Mustakabali wa soka duniani lazima uamuliwe kupitia mashauriano, majadiliano ya pamoja na heshima kwa mifumo iliyowekwa ya uongozi wa mchezo wetu," alisema Sheikh Salman.

    Vyama 55 wanachama wa soka barani Ulaya, UEFA, vilipiga kura Alhamisi wiki hii kususia Kombe la Dunia ikiwa mpango huo ungelitekelezwa.

    Soma zaidi:

  5. Marekani na Israel zinajiandaa kushambulia tena miundombinu ya nishati ya Iran - ripoti

    Trump na Netanyahu

    Chanzo cha picha, Getty Images

    CBS News, mshirika wa habari wa BBC linaripoti Marekani na Israel zinapanga operesheni dhidi ya miundombinu ya nishati Iran, na huenda mashambulizi hayo yakatekelezwa mapema wiki ijayo.

    Kwa mujibu wa vyanzo vilivyonukuliwa na CBS, Rais wa Marekani Donald Trump bado hajatoa amri ya mwisho ya kuanzishwa kwa mashambulizi hayo.

    Mtandao huo ulisema kuwa operesheni hii itakuwa mojawapo ya mashambulizi makali zaidi kufanywa dhidi ya Iran katika vita vya Marekani na Israel.

    Kituo hicho kilibainisha kuwa kulikuwa na majadiliano kuhusu kukomesha mashambulizi kabla ya masoko ya fedha kufunguliwa siku ya Jumatatu.

    Baadaye, mwandishi wa Axios alimnukuu afisa mmoja wa ngazi ya juu wa Marekani akisema kuwa "Rais Trump anafikiria kuamuru kupigwa kwa mitambo ya nishati ya Iran katika siku zijazo, lakini bado hajatoa amri ya mwisho ya kuitekeleza."

    Soma pia:

  6. Natumai hujambo.