Lionel Messi mfungaji bora wa muda wote kwenye Kombe la Dunia

Chanzo cha picha, Robbie Jay Barratt - AMA/Getty Images
Nahodha wa Argentina, Lionel Messi, alifunga mabao mawili katika mechi ya pili ya Kundi J ya Kombe la Dunia dhidi ya Austria, na kuiongoza Argentina katika ushindi wa mabao 2-0.
Messi, ambaye pia alikosa penalti mapema katika mchezo huo, alifunga mabao yake katika dakika ya 38 na dakika ya 90+5, na kuhakikisha timu yake inapata ushindi muhimu.
Nyota huyo wa Argentina, ambaye atatimiza miaka 39 tarehe 24 Juni, anaendelea kuweka historia kama mfungaji bora wa muda wote katika fainali za Kombe la Dunia, akiwa amefunga mabao 18 katika mechi 28 alizocheza.
Baada ya Messi katika orodha hiyo ni Miroslav Klose wa Ujerumani na Kylian Mbappe wa Ufaransa, ambao kila mmoja ana mabao 16. Nafasi inayofuata inashikiliwa na Ronaldo wa Brazil mwenye mabao 15.
Ushindi huo umeimarisha nafasi ya Argentina katika Kundi J huku Messi akiendelea kuonesha ubora wake licha ya umri wake mkubwa katika soka la kimataifa.
Lionel Messi, ambaye amefunga mabao yote matano ya Argentina katika Kombe la Dunia 2026 hadi sasa, pia amesawazisha rekodi ya kufunga mabao katika mechi sita mfululizo za mashindano hayo.
Messi sasa anajiunga na nyota wengine wawili wa soka waliofanikiwa kuweka rekodi hiyo: Just Fontaine wa Ufaransa na Jairzinho wa Brazil, ambao walifanya hivyo katika Kombe la Dunia la mwaka 1958.
Unaweza kusoma;

















