Moja kwa moja, Mazungumzo ya Marekani na Iran kuanza Uswisi

Jumamosi jioni, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, aliondoka Washington kuelekea Uswisi kwa ajili ya mazungumzo hayo

Skip Video and continue reading
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Mazungumzo ya Marekani na Iran kuanza Uswisi huku Tehran ikidai kufunga Mlango-Bahari wa Hormuz

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mazungumzo ya Marekani na Iran kuanza Uswisi huku Tehran ikidai kufunga Mlango-Bahari wa Hormuz

    Mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Marekani na Iran yanatarajiwa kuanza nchini Uswisi licha ya jeshi la Iran kusema kuwa limefunga tena Mlango-Bahari wa Hormuz kufuatia mashambulizi ya Israel kusini mwa Lebanon.

    Jeshi la Marekani limepinga madai hayo, likisema kuwa "usafiri wa meli unaendelea kama kawaida". Iran ilisema kuwa Mlango-Bahari wa Hormuz ulifungwa kujibu mashambulizi mabaya ya Israel nchini Lebanon, ambayo Tehran ilisema yalikiuka makubaliano yake na Marekani ya kumaliza vita.

    Jumamosi jioni, Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, aliondoka Washington kuelekea Uswisi kwa ajili ya mazungumzo hayo.

    Ujumbe wa Iran unaojumuisha Spika wa Bunge, Mohammad Bagher Ghalibaf, na Waziri wa Mambo ya Nje, Abbas Araghchi, tayari umewasili.

    Duru mpya ya mazungumzo inatarajiwa kuanza Jumapili. Vance alisema ana matumaini ya kupiga hatua “kuhusu suala la nyuklia” na pia “suala la usitishaji mapigano nchini Lebanon”.

    Akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kupanda ndege yake, aliulizwa kuhusu mapigano kati ya Israel na Hezbollah pamoja na mashambulizi ya anga ya Israel kusini mwa Lebanon.

    "Hali kwa kweli inaendelea kuimarika zaidi huko, na mambo yanaanza kutulia kidogo," Vance alisema.

    "Hili ni jambo ambalo tutalazimika kuendelea kulisimamia ili kuhakikisha kwamba Israel na Lebanon zote mbili ziko salama na zenye usalama. Hilo ndilo lengo kuu — kufanya eneo lote liwe salama na utulivu," Vance aliongeza.

    Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmail Baghaei, alisema kuwa nchi yake itakuwa "ikisisitiza upande mwingine kutimiza ahadi zake."

    Soma zaidi:

  2. Hujambo na karibu katika matangazo yetu Mubashara.