Kombe la Dunia 2026: Saudi Arabia walazimishwa sare na Uruguay

Chanzo cha picha, Getty Images
Saudi Arabia wamelazimishwa sare ya 1-1 na Uruguay waliosawazisha dakika ya 80 baada ya Saudia kuongoza dakika ya 41 ya mchezo huo uliopigwa usiku wa manane.
Mapema usiku wawakilishi wa Afrika Misri walitoshana nguvu na Ubelgiji kwa sare ya goli 1-1.
Misri waliongoza katika dakika ya 20 kupitia kwa Emam Ashour aliyeachia mkwaju mkali baada ya pasi safi ya Mohamed Salah.

Chanzo cha picha, Reuters
Ubelgiji walisawazisha dakika ya 66 baada ya mlinzi wa kulia wa Misri Mohamed Hany kujifunga katika harakati za kuokoa.
Mapema zaidi, Cape Verde waliiwakilisha Afrika na kushangaza dunia baada ya kuonesha mbinu za hali ya juu za ulinzi na kutoka sare ya bila kufungana na Hispania ambao ni mabingwa wa dunia wa mwaka 2010 na mabingwa wa sasa wa Ulaya huku mlinda lango wa Cape Verde, Vozinha mwenye umri wa miaka 40 akijizolea sifa kemkem kwa umahiri wake.
Alibubujikwa na machozi baada ya kipenga cha mwisho.
Pia unaweza kusoma:
















