Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Marekani inaendelea na Mazungumzo na Iran huku mashambulizi yakisitishwa - Trump

Hata hivyo, ameonya kuwa iwapo mazungumzo hayo hayatakuwa na mafanikio, Marekani "itarejea kufanya kile tulichokuwa tukifanya" kabla ya kusitishwa kwa mashambulizi.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Moto wa nyika: Macron asema Ufaransa inakabiliwa na hali mbaya zaidi tangu Vita vya Pili vya Dunia

    Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ameahidi kutumia kila rasilimali iliyopo kupambana na moto mkubwa wa nyika unaoendelea nchini humo akisema janga hilo ni mbaya zaidi kuwahi kuikumba Ufaransa tangu Vita vya Pili vya Dunia.

    Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ameonya kuwa hali itaendelea kuwa ngumu zaidi alipokuwa akitembelea kituo cha operesheni za kuzima moto katika eneo la Gironde, ambalo limeathiriwa vibaya na moto huo uliosababisha mioto mikubwa isiyoweza kudhibitiwa.

    Akizungumza na vikosi vya zimamoto na wahudumu wa dharura, Macron alisema:

    "Tunakabiliwa na hali ngumu zaidi kuwahi kushuhudiwa, hali ambayo haijawahi kutokea tangu Vita vya Pili vya Dunia."

    Aliongeza kuwa msimu wa moto wa nyika, ambao kwa kawaida hufikia kilele mwezi Agosti, bado haujaanza kikamilifu.

    Rais Macron ameonya kuwa viwango vya joto vinatarajiwa kupanda tena, akisisitiza kuwa cha msingi kwa sasa ni kuokoa maisha.

    Wakati huo huo, wazima moto nchini Uhispania wamekuwa wakipambana kudhibiti baadhi ya moto mbaya zaidi wa nyika katika historia ya hivi karibuni ya nchi hiyo huku kukiwa na onyo la wimbi kubwa la joto linaloongezeka ambalo linaweza kuzorotesha zaidi hali hiyo.

    Viwango vya joto katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo vinatarajiwa kuwa ya juu zaidi.

    Waziri Mkuu, Pedro Sanchez, ameonya kuwa ni wakati mgumu kwa nchi yake huku akitoa wito kwa vyama vya kisiasa kuweka kipaumbele katika kuunda mkataba wa kitaifa wa dharura wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

    Soma Zaidi:

  2. Johnson & Johnson yajitolea kulipa hadi $5.5bn kumaliza kesi za poda ya watoto

    Kampuni ya Johnson & Johnson (J&J) imejitolea kulipa hadi dola bilioni 5.5 (pauni bilioni 4.14) ili kumaliza maelfu ya kesi zinazodai poda yake ya watoto pamoja na bidhaa nyingine zenye madini ya talcum husababisha saratani ya ovari au kifuko cha mayai.

    Makubaliano hayo makubwa yanakusudia kumaliza mzozo wa kisheria uliodumu kwa miaka kadhaa na kuendelea kuigharimu kampuni hiyo kubwa ya huduma za afya nchini Marekani.

    J&J imeendelea kusisitiza kuwa bidhaa zake zenye talcum hazisababishi saratani, na tayari imebadilisha viambato vya poda yake ya watoto inayotumiwa na watu wengi.

    Makamu wa Rais wa masuala ya kesi za kisheria wa kampuni hiyo, Erik Haas, alisema Jumatatu kuwa madai hayo "hayana msingi", na kwamba J&J imeamua kufikia makubaliano ili kutatua kabisa suala hilo.

    Kampuni hiyo imesema makubaliano hayo yatahusisha takriban kesi 69,000, ambazo ni sehemu kubwa ya madai yaliyosalia yanayohusiana na bidhaa za talcum. J&J imeeleza kuwa italipa hadi dola bilioni 3 mwaka ujao, na kusitarajiwe malipo mengine kabla ya mwaka 2028.

    J&J pia imesema pendekezo hilo litalazimika kukubaliwa na kampuni za mawakili zinazowawakilisha asilimia 95 ya walalamishi wa kesi za saratani ya ovari katika mahakama za majimbo na za shirikisho, kabla ya makubaliano hayo kukamilika.

    Katika taarifa yake, Haas alisema kampuni ina imani kuwa ingeibuka mshindi endapo kesi hizo zingeendelea mahakamani, kama ilivyofanikiwa katika kesi nyingi ambazo tayari zimeamuliwa.

    Aliongeza kuwa makubaliano hayo yataiwezesha kampuni kuhitimisha suala hilo na kuelekeza nguvu zake katika jukumu lake la kutengeneza dawa na vifaa vya tiba vinavyookoa maisha.

    Soma Zaidi:

  3. Mazungumzo ya vita vya Iran yanaendelea huku mashambulizi yakisitishwa - Trump

    Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa kuna "mazungumzo ya kirafiki yanayoendelea" kuhusu mzozo wa Iran, baada ya pande zinazopigana kutoshambuliana kwa siku ya tatu mfululizo.

    Akiwa ndani ya ndege ya Air Force One siku ya Jumatatu, Trump alieleza matumaini yake kwamba vita hivyo vinaweza kufikia mwisho. Aliwaambia waandishi wa habari: "Ninaamini kuna uwezekano mkubwa jambo fulani likatokea."

    Alionyesha matumaini kwamba vita vinaweza kumalizika Jumatatu, akiwaambia waandishi wa habari ndani ya ndege ya Air Force One: "Nafikiri kuna fursa nzuri ya kutokea kwa jambo fulani."

    Hata hivyo, alionya kuwa iwapo mazungumzo hayo hayatakuwa na mafanikio, Washington "itarejea kufanya kile tulichokuwa tukifanya" kabla ya kusitishwa kwa mashambulizi.

    Kwa upande wake, Tehran imekanusha kuwa kuna mazungumzo yoyote ya moja kwa moja yanayoendelea.

    Trump alisema aliamua kusitisha mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran siku ya Ijumaa baada ya nchi zinazosaidia kupatanisha pande hizo kumwomba kutoa fursa nyingine kwa mazungumzo.

    Iran pia imesitisha mashambulizi yake.

    Hatua hiyo inafuatia karibu wiki mbili za mashambulizi ya kila siku ya Marekani na ya kulipizana kisasi kati ya pande hizo, hali iliyovuruga kwa kiasi kikubwa makubaliano ya usitishaji mapigano yaliyofikiwa mnamo mwezi Juni.

    Wakati huo, jeshi la Marekani lilisema mashambulizi yake yalilenga kupunguza uwezo wa Iran wa kuhatarisha usafirishaji wa meli za kibiashara katika Mlango Bahari wa Hormuz, ambao ni njia muhimu duniani ya usafirishaji wa mafuta.

    Soma Zaidi Hapa:

  4. Hujambo Msomaji wetu. Karibu katika matangazo yetu mubashara tarehe ni 28/07/2026.