Moto wa nyika: Macron asema Ufaransa inakabiliwa na hali mbaya zaidi tangu Vita vya Pili vya Dunia

Chanzo cha picha, EPA/Shutterstock
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ameahidi kutumia kila rasilimali iliyopo kupambana na moto mkubwa wa nyika unaoendelea nchini humo akisema janga hilo ni mbaya zaidi kuwahi kuikumba Ufaransa tangu Vita vya Pili vya Dunia.
Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, ameonya kuwa hali itaendelea kuwa ngumu zaidi alipokuwa akitembelea kituo cha operesheni za kuzima moto katika eneo la Gironde, ambalo limeathiriwa vibaya na moto huo uliosababisha mioto mikubwa isiyoweza kudhibitiwa.
Akizungumza na vikosi vya zimamoto na wahudumu wa dharura, Macron alisema:
"Tunakabiliwa na hali ngumu zaidi kuwahi kushuhudiwa, hali ambayo haijawahi kutokea tangu Vita vya Pili vya Dunia."
Aliongeza kuwa msimu wa moto wa nyika, ambao kwa kawaida hufikia kilele mwezi Agosti, bado haujaanza kikamilifu.
Rais Macron ameonya kuwa viwango vya joto vinatarajiwa kupanda tena, akisisitiza kuwa cha msingi kwa sasa ni kuokoa maisha.
Wakati huo huo, wazima moto nchini Uhispania wamekuwa wakipambana kudhibiti baadhi ya moto mbaya zaidi wa nyika katika historia ya hivi karibuni ya nchi hiyo huku kukiwa na onyo la wimbi kubwa la joto linaloongezeka ambalo linaweza kuzorotesha zaidi hali hiyo.
Viwango vya joto katika baadhi ya maeneo ya nchi hiyo vinatarajiwa kuwa ya juu zaidi.
Waziri Mkuu, Pedro Sanchez, ameonya kuwa ni wakati mgumu kwa nchi yake huku akitoa wito kwa vyama vya kisiasa kuweka kipaumbele katika kuunda mkataba wa kitaifa wa dharura wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Soma Zaidi:





















