Meli yenye bendera ya Tanzania yakamatwa na maharamia Somalia

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Meli ya wafanyabiashara yenye bendera ya Tanzania imekamatwa na maharamaia wa Somalia katika Ghuba ya Aden.
Meli hiyo kwa jina MT Asana ina mafuta na kemikali na ilikuwa na wafanyakazi 20, wanane kutoka Ujerumani na 10 kutoka Ufilipino.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Ujerumani ilisema kama kanuni yake, haitoi maoni kuhusu matukio ya raia wa Ujerumani kutekwa nyara nje ya nchi.
Shirika la United Kingdom Maritime Trade Operations (UKMTO) lilisema wiki iliyopita kuwa meli iliyovamiwa na watu wasioidhinishwa katika Ghuba ya Aden ilikuwa imeelekezwa kuingia katika maji ya Somalia, na tukio hilo lilitambuliwa rasmi kama utekaji wa meli.
Maharamia wa Somalia walisababisha machafuko makubwa katika maji yaliyoko kando ya pwani ya nchi hiyo katika Pembe ya Afrika kati ya mwaka 2008 na 2018.
Baada ya kipindi cha utulivu, shughuli za uharamia zilianza kuongezeka tena mwishoni mwa mwaka 2023.



























