Ghana yaunga mkono muhula wa miaka mitano kwa Rais

Chanzo cha picha, Reuters
Serikali ya Ghana imekubali pendekezo la kuongeza muda wa muhula wa urais kutoka miaka minne hadi miaka mitano, Waziri wa Sheria wa taifa hilo la Afrika Magharibi amesema siku ya Alhamisi.
Rais John Dramani Mahama aliunda kamati mwaka jana kupitia upya Katiba ya mwaka 1992 na kutoa mapendekezo mbalimbali, ambayo baadhi yake yamekubaliwa na serikali.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Waziri wa Sheria, Dominic Ayine, alisema kuwa muhula wa Bunge pia utaongezwa ili uendane na muhula mpya wa rais wa miaka mitano.
Aidha, serikali imeunga mkono pendekezo la kupunguza umri wa chini wa kugombea urais kutoka miaka 40 hadi miaka 35, hatua inayolenga kutoa nafasi kubwa zaidi kwa viongozi vijana kushiriki katika uongozi wa taifa.
Serikali pia imekubali kimsingi pendekezo la kamati la kupunguza umri wa chini wa wagombea urais, ambao kwa sasa ni miaka 40. Hata hivyo, imefanyia marekebisho pendekezo hilo kwa kuweka umri huo kuwa miaka 35 badala ya miaka 30 kama ilivyopendekezwa awali na kamati.
Hatua hiyo inalenga kupanua ushiriki wa vijana katika uongozi wa juu wa taifa huku ikiendelea kuhakikisha kuwa wagombea wa urais wanakuwa na kiwango cha kutosha cha uzoefu na ukomavu wa kisiasa.
Pia unaweza kusoma:



























